Kamusi ya wanafunzi ya Kiswahili – kiingereza ni kamusi inayowalenga wanafunzi wa ligha zote mbili ambao hawajapata umilisi kamili wa lugha mojawapo au ambao ndio kwanza wanaanza kujifunza Kiswahili. LLi kutimiza lengo hili, kamusi hii inayosisitiza ‘uwili lugha’ imepangwa kwa ustadi mkubwa ili kuwapa wasomaji wake msamiati wa msingi wa lugha zote mbili; ikianza na Kiswahili ambayo ndiyo lugha kuu ya mawasiliano (Lingua Franka) ya watu wa Afrika Mashariki na eneo la maziwa makuu.
Mpangilio wa vidahizo, tafsiri na maelezo na mifano ya matumizi ya vidahizo katika sentensi ni nakshi inayoamsha hamu ya msomaji mara moja. Katika mpangilio huu, maelezo na msamiati wa msingi wa lugha hizi mbili, ikianza na kidahizo katika Kiswahili, kategoria ya neon, (yaani: kitenzi, kivumishi, kielezi n.k), ngeli (katika nomino), kasha kisawe cha kiingerez